WELCOME ALL

Gonga Hapa.

Tuesday, April 30, 2013

Maisha ni kusaidiana

WELCOME TO KUNAMBI BLOG!!!

Suala la Maisha ni kusaidiana na si eti kwa sababu mwanamke ameolewa basi baba unakua mtu wa kutoa amri tu ndani ya nyumba,hiyo hapana kuna mda mwengine mama nae anakua kachoka pia so yatupasa kina baba kuelimika na kusaidia wake zetu


hapo zamani ilikua ikisadikika kua mwanamke ni chombo cha starehe tu lakini si sahihi kwa sababu mwanamke ndio mlezi mkuu wa familia nzima,sasa basi yatupasa kuwapenda,kuwaheshimu,kuwatunza na kuwasaidia pia.

TRUST YOUR SELF

WELCOME TO KUNAMBI BLOG!!!
Maisha ya sasa katika suala zima la mapenzi yamekua ya kusuasua sana kiasi kupeleka wanandoa au wapenzi kusaliatiana na baadae kuleta ugomvi na masikilizani hasi kwenye mahusiano.







Kufuatia hali hiyo mchekeshaji mahiri na msanii wa filamu Hollywood nchini marekani Willy Smith aliongea maneno hayo.
WELCOME TO KUNAMBI BLOG!!! Kufuatia vurugu kubwa zilizozuka mkoani Lindi wilaya ya Liwale kwa wakulima wa korosho kudai mafao yao ya shilingi mia sita (600) imesababisha tafrani kubwa kiasi nyumba ya mbunge wa wilaya hiyo kuchomwa kwa moto na kuharibiwa vibaya, na baadhi ya magari kuchomwa moto.




kufuatia vurugu hizo serikali ya kijiji iliamriwa na mamlaka ya bodi ya korosho kumalizia kiasi hicho kinachodaiwa na wakulima ili kuepusha vurugu wilayani humo
WELCOME TO KUNAMBI BLOG!!!
inasadikika watoto wadogo hawawezi kudhuriwa na viumbe hatari kama nyoka,kwani wanapata ibra kutoka kwa mungu,malaika hawa wa mungu hulindwa na nguvu za mungu kwenye hatari ya aina yoyote ile,lakini kinachotakiwa unapomkuta mtoto kwenye hatari hutakiwi kushtuka wala kupiga mayowe kwani kwa kufanya hivyo utamshtua kiumbe hatari aliye karibu nae kuweza kumdhuru,lakini kama utakua na roho ngumu na kutulia kimya huyo kiumbe hatari kama vile nyoka n.k anaweza kucheza na mtoto kisha akaondoka zake bila kumdhuru.

Tuesday, October 18, 2011

Viumbe Hatari Kabisa Duniani, Anayeshika Namba Moja Ni Mbu!

Simba, Nyati, Faru, Chatu....haya ndiyo majina ya wanyama yanayoweza kukujia akilini pindi ukiulizwa MNYAMA YUPI NI HATARI ZAIDI KWA MWANADAMU. Well, amini usiamini, kiumbe hatari zaidi ni mdogo mara elfu kadhaa akilinganishwa kiumbo na hao majabali tunaowafahamu. Na udogo wake si katika umbile pekee bali pia hata sauti yake ni ndogo kulinganisha na mbwa, paka au mbuzi, achilia mbali wababe kama Simba, Chui au Faru. Kiumbe huyo hatari wa kuogopwa kwa gharama yoyote ile ni MBU.
Kwa mujibu wa takwimu, Mbu ni kiumbe hatari zaidi kuliko wote duniani. Kiumbe huyo hatari ni maarufu kwa kuambukiza rundo la magonjwa, kubwa zaidi ikiwa ni homa ya malaria. Lakini pia mbu hueneza homa ya matende (elephantiasis), homa ya manjano (yellow fever), kindiga popo (dengue fever) na homa ya Mto Nile.

KESI DHIDI YAKE: Mbu anawajibika kusababisha kati ya vifo milioni 2 hadi 3 kwa mwaka.

VIJIWE (Hangout) VYAO: Takriban dunia nzima lakini zaidi barani Afrika, Asia na Amerika ya Kaskazini.

ANAVYOSABABISHA MAAFA: Mbu huambukiza maradhi ya kuuma kwenye ngozi ya binadamu na kumwaga mate yake yenye vijidudu vinavyosababisha homa husika. Ukiweka kando vipele vidogo vinavyotokea mahala alipouma mbu, anayeambukizwa na mbu hatambua maambukizo hadi pale kinga za mwili inaposhtuka (na kuleta dalili mbalimbali).

JINSI YA KUMKWEPA: Njia ya kupambana na mbu na maambukizo ni pamoja na kutumia chandarua kilichomwagiwa kinga, kuangamiza sehemu za mazalio ya mbu na vidonge vya kinga.
------------------------------------------------------------------------------------------

Nyoka Wenye Sumu Kali
Japo kuna zaidi ya aina 2,000 za nyoka, 450 kati yao wenye sumu,ni aina 250 tu kati yao ndio wenye uwezo wa kuua binadamu.

KESI DHIDI YAO: Nyoka wenye sumu kali husababisha kati ya vifo 50,000 na 250,000 kwa mwaka.

VIJIWE VYAO: Zaidi ni Afrika,Asia na Amerika ya Kaskazini

WANAVYOSABABISHA MAAFA: Nyoka wana kasi sana na sehemu yoyote katika mwili wa binadamu inaweza kuwa kugongwa na kiumbe huyo hatari.Lakini ni hatari zaidi nyoka anapomgonga mtu kwenye mshipa wa damu kwani hiyo huharakisha kusambaa kwa sumu ya kiumbe huyo.Nyoka hutumia sumu yao kumlegeza mtu na pengine kumpotezea fahamu.Majoka makubwa kama Mfalme Kobra (King Cobra) yanaweza kusimama hadi usawa wa kichwa cha binadamu,huku wengine wakiweza kutema na kurusha sumu yao kutoka mbali kwenda kwenye macho ya mwanadamu.

JINSI YA KUWAKWEPA: Mara nyingi nyingi nyoka hushambulia pale tu pale anapobughudhiwa.Kwahiyo ushauri muhimu wa kuepuka shambulizi kutoka kwa viumbe hao ni kujiepusha nao (Stay away!).Pia ni muhimu kuvaa mabuti kwenye mazingira yanayoweza kuwa na nyoka.Epuka mapori yanayoweza kuwa makazi ya nyoka.Na ikitokea umeomwona nyoka,inashauriwa urudi kinyumenyume taratibu kwani anaweza kujirusha mara nusu ya urefu wake,na mtikisiko kidogo tu unaweza kumasha hasira za kiumbe huyo hatari.
--------------------------------------------------------------------------------------------
Nge


Ni kiumbe hatari mwenye sura mbaya maradufu.Inaaminika kuwa ng'e anaweza kuwa anasababisha vifo vingi zaidi ya vile vinavyorekodiwa rasmi,sababu ya kuhisi hivyo ikiwa ni mazingira wanayoishi viumbe hao na ugumu wa kupatikana tiba dhidi ya sumu yao.Hata hivyo,japo kuna aina tofauti 1500 za ng'e ni 25 tu kati yao ambao ni hatari kwa uhai wa uhai wa binadamu.

KESI DHIDI YAO: Ng'e husababisha kati ya vifo 800 hadi 2,00 kwa mwaka

VIJIWE VYAO: Duniani kote hususan Afrika,America ya Kusini na Kaskazini na Asia ya Kati.

WANAVYOSABABISHA MAAFA: Ng'e humlegeza binadamu baada ya kumdunga sumu kwa kutumia "vijisindano" vilivyopo kwenye mikia yao.Kama ilivyo kwa sumu nyingine za wadudu/wanyama,binadamu walio hatarini zaidi ni wale wenye aleji,japo ng'e wengi wenye sumu wanaopatikana Afrika wanaweza kumdhuru mtu yeyote yule.

JINSI YA KUWAKWEPA: Ng'e huwa active zaidi nyakati za usiku na hupendelea kujipumzika mchana.Kwahiyo ni muhimu kuhakikisha sehemu ya kujilaza ipo salama kabla ya kuubwaga mwili.Kadhalika ni muhimu kupunga mavazi na/au soksi kuhakikisha hakuna ng'e humo,vinginevyo itakuwa balaa.
----------------------------------------------------------------------------------------------
WENGINEO KWA KIFUPI
Paka Wakubwa (Simba,Chui,nk)

Paka Wakubwa (kwa mfano yaani Simba,Chui,nk) husababisha takriban vifo 800 kwa mwaka
...............................................................................................
Mamba
Mamba husababisha kati ya vifo 600 na 800 kwa mwaka
............................................................................................
Tembo
Pamoja na upole wao,Tembo husababisha kati ya vifo 300 na 500 kwa mwaka
.............................................................................................
Kiboko
Mwamba huyo wa majini mwenye sura mbaya husababisha vifo kati ya 100 na 150 kwa mwaka
..............................................................................................
Konyeza (jellyfish
Kiumbe huyu wa baharini husababisha takriban vifo 100 kwa mwaka
..............................................................................................
Papa
Kiumbe huyu hatari wa baharini husababisha takriba vifo 100 kwa mwaka
...............................................................................................
Panda
Husababisha kati ya vifo 5-10 kwa mwaka
***********************************************************************************************

Sunday, October 16, 2011

KITUKO CHA KARNE

MWANAMKE mkazi wa kijiji cha Ikandamoyo, wilayani hapa, Veronica Saleh ‘Mama Kaela’ (50), amefanya uamuzi adimu wa kuolewa na wanaume wawili ambao anaishi nao kijijini hapo.

Kijiji hicho kipo umbali wa takribani kilometa 30 kutoka mjini hapa katika Jimbo la Katavi linalowakilishwa na Waziri Mkuu Mizengo Pinda.

Pamoja na ndoa hiyo iliyowezeshwa na mume mkubwa kukubali kuishi na mume mdogo, imeelezwa kuwa mwanamke huyo ndiye ‘aliyewaoa’ wanaume hao kwa zaidi ya miaka saba sasa, huku akiwa na amri kuu katika nyumba, kama ilivyo katika ndoa za kawaida.

Wanaume hao ni Paulo Sabuni ‘Baba Kaela’ (60) ambaye ndiye mume mkubwa na Arcado Mlele (45) ambaye ni mume mdogo.

Taarifa za kuwapo kwa ndoa hiyo ya aina yake, zililifikia gazeti hili na kufanyiwa uchunguzi kwa zaidi ya wiki tatu, na hatimaye katikati ya wiki hii, wahusika walikubali wao wenyewe kuzungumzia suala hilo. Kwa mujibu wa maelezo ya mwanamke huyo ambaye alionekana kuwa msemaji wa familia hiyo, yeye na mumewe mkubwa, walifika kijijini hapo miaka 24 iliyopita, wakitoka kijiji cha Usumbwa mpakani mwa Chunya, Mbeya na Tabora.

Wakiwa kijijini hapo mume wake aliendelea kufanya kazi ya ukulima wakati yeye mama (Veronica), pamoja na kilimo hujihusisha na upishi na uuzaji wa pombe ya kienyeji ya iitwayo kayoga.

Mwanamke huyo ambaye amesema ana watoto wanne, Alfred (20), binti mwenye miaka 16 (ambaye ameolewa) na wengine wawili wa kiume, mmoja akisoma darasa la sita na mdogo ana miaka saba, amesema hana shida na waume wake.
Ingawa wanandoa hao walizungumza kwa hadhari, majirani walikiri kuwa mwanamke huyo anaishi na wanaume hao wawili kwa amani na kwamba mwanamke huyo ndiye mwenye sauti na si waume zake.

“Si siri tena sasa, tumeshawazoea, kwani wanaishi kwa amani ila yule mume mdogo anaishi kwenye nyumba aliyoachiwa na marehemu baba yake, lakini anashinda kwa mume mkubwa, ambapo inajulikana kijijini hapa kuwa ni nyumba kubwa. “Basi pale ni mambo yote, kula na kunywa, mama huyu amewapangia zamu wanaume hao kama afanyavyo mume mwenye wake wengi. Ama kweli ukistaajabu ya Musa utaona ya Firauni,” alisema mkazi mmoja kwa masharti ya jina lake kutoandikwa gazetini. Ilielezwa, kwamba wanaume hao wana akili timamu na hawatumii kilevi cha pombe kama ilivyo kwa mke wao.

Hata hivyo, mume mkubwa anapewa sifa za upole tofauti na mume mdogo anayetajwa kuwa mkorofi kiasi cha mara kadhaa kumchapa makofi mkewe anapomuudhi.

Majirani wanadai kwamba Mama Kaela na mumewe Paulo, walipofika kijijini hapo, walipokewa na kuishi maisha ya kawaida, lakini baadaye mama huyo alianza kuwa na uhusiano wa kimapenzi na Arcado, ambaye naye alilazimika kuachana na mkewe wa ndoa anayefahamika kijijini hapo kwa jina la Mama Pere.

Ilielezwa na mashuhuda hao kwamba mume mkubwa alipobaini uhusiano huo, alikuja juu, lakini mwanamke huyo inadaiwa alimweleza mumewe huyo, atake asitake lazima wataishi wawili, vinginevyo ataachana naye, ndipo mume mkubwa alipokubali kuishi na mume mwenza.

Katika maisha ya kawaida katika familia hiyo, inaelezwa kwamba katika baadhi ya siku ikitokea kuwa mama huyo amechoka kupika, mume mdogo huchukua jukumu la kupika na kumwandalia chakula na maji ya kuoga mume mkubwa.

“Lakini mara nyingi kwa mfano, ikiwa ni zamu ya mama huyo kulala kwa mumewe mkubwa, basi humfulia nguo zake kisha anakwenda kwa mumewe mdogo nako anamfulia nguo.

“Ndivyo wanavyoishi, nasi sasa tumewazoea ila yule mama ni mkali na ana sauti pale kwake kwa wanaume wale ila tunaona kama ana wivu sana kwa huyu mdogo ambaye naye pia ana wivu kwa mkewe huyo, labda anahofia kuwa mama huyo anaweza kuongeza mwanamume mwingine,” anasema mmoja wa majirani hao.

Hakuna mazuri yasiyokuwa na machungu, japo familia hiyo inaelezwa kuwa na amani, mtoto wao mdogo nusura avuruge uhusiano wa wanandoa hao, baada ya kuibuka mzozo wakati wa maandalizi ya ubatizo wake.

Kwa sababu anazojua mama, ingawa inafahamika kuwa wote ni watoto wa mume mkubwa, mke huyo katika hati za ubatizo aliandikisha ubini wa mtoto huyo kuwa ni Mlele (akimaanisha kuwa mtoto wa mume mdogo), lakini mume mkubwa aliweka pingamizi kanisani akidai yeye ndiye baba halali wa mtoto huyo.

Kwa mujibu wa mwanamke huyo, yeye na Arcado ni waumini wa madhehebu ya Katoliki wakati Paulo ni Mpentekoste. Madai ya mzozo wa uhalali wa `ubaba’ wa mtoto huyo, yalithibitishwa na baadhi ya wakazi wa kijiji hicho, akiwamo mwalimu wa dini wa Kigango cha Kanisa Katoliki Uruira, Mashaka Abel. Walisema miaka sita iliyopita, mtoto huyo akiwa na umri wa mwaka mmoja, alifanyiwa taratibu za ubatizo, lakini ilishindikana, kutokana na wanaume hao, kila mmoja kudai ndiye baba mzazi wa mtoto.

“Lilikuwa jambo la kustaajabisha sana, kwani familia hiyo ilifanya maandalizi yote ya sherehe ya ubatizo wa mtoto huyo, lakini siku hiyo kanisani wakati huo ilikuwa ni kigango cha Katumba ambacho sasa ni Uruira, sakata lilianzia pale Padri alipomwuliza mama wa mtoto huyo ubini wa mtoto naye akasema ni Mlele.

“Hapo ndipo mume mkubwa alipopinga na kudai kuwa mtoto yule si wa Arcado bali wake na yeye ndiye baba halali. Padri hakuamini, aliuliza tena na tena na majibu yakawa ni yale yale, ndipo ubatizo ukashindikana,” alisema Katekista Abel.

Kazi ya kutafuta undani wa ndoa hiyo haikuwa rahisi kutokana na mazingira ya woga na usiri uliokusudiwa kubaki, ambapo awali mama alisema kwamba mume wake ni Paulo pekee japo siku ambayo mwandishi wa habari hizi alifika kijijini hapo na baadaye nyumbani kwa wanandoa hao na kumkuta mume mdogo (Arcado akimsaidia mkewe kukoroga pombe. Awali katika utambulisho, walidai kuwa ni mtu na mdogo wake na kusita kuzungumzia maisha yao ya kifamilia.

Mke wao ambaye alionekana wazi kuwa ni msemaji mkuu alifoka na kuja juu, akidai kuwa hayuko tayari kuzungumzia uhusiano wake na wanaume hao wawili, ingawa alikiri kuwa wanaishi pamoja.

"Kwa hiyo umefunga safari yote hii kutoka huko ulikotoka ili uje kwangu mie Veronica … nasema sitaki kabisa mtu kuja hapa na kutaka kunivurugia mpangilio wa maisha yangu, kwanza nani alikueleza hayo, wambea wakubwa hao yanawahusu nini watu hao?” alihoji.

“Mie mume wangu ni huyu Paulo basi … sasa leo umeniachia vurugu ndani ya nyumba nitapigwa na huyo mume wangu Paulo, kwani mmenishikisha ugoni?” alifoka Mama Kaela. Hata hivyo, mume mkubwa alidai kuwa hatamwadhibu mkewe huyo na kwamba wataendelea kuishi pamoja na mdogo wake Arcado kwa amani. Hata hivyo, akina mama wengi kijijini hapo wanalaani kitendo cha mama huyo kuishi na wanaume wawili ambapo waliomba uongozi wa Kanisa uingilie kati, ili mama huyo aweze kufunga ndoa na mume mmoja.

Lakini kwa upande mwingine, baadhi walimpongeza mwanamke huyo wakidai kuwa kitendo hicho ni cha kijasiri kwa mwanamke, kumudu kuishi na wanaume wawili na kuwa na mamlaka juu yao.

Thursday, October 13, 2011

CHATU

Kiumbe huyu...Chatu(Python) ndo kati ya nyoka wachache duniani wenye meno zaidi ya 2 maana hawana sumu. Meno yao hutumika kukamata msosi mdoni na kuubana ili usikimbie. wanaua kwa kubana na kujizungusha kwa mnyama kumziba pumzi na kuvunja vunja mbavu na mifupa. Hapa alimeza Impala (Swala pala) . bahati mbaya akanasa kwenye fensi ya umeme..South border to Botswana...wadau wakamdaka akikata roho....Follow...
Hapa ameona fensi ndo nuksi akaamua king'ata kumbe ndo anapigwa shoti zaidi

Mnyama mwenewe aliyemeza anasazi kama hii hapa...alafu mtamu kuliko mbuzi,anaitwa mbawala kwa waliowahi tembelea mbuga za wanyama watakua wanamfahamu vizuri


Wadau walimchinja wakapata mboga mbili tofauti...nyama choma ya swala na mapande ya chatu ya kumwaga...Yummy!!



Huyu(sio chatu) alimeza yai kubwa la Mbuni (Ostrich). Hapo najiuliza je Nazi imeingiaje kwenye tumbo la nyoka!! viumbe hawa wamepewa uwezo wa kula vitu vikubwa sana kuliko hata maumbile yao lakini lazima waishi na lazima wale.


akameza yai linye ukubwa kama picha inavyoonyesha hapo chini

Simba Sports Club-Tanzania



Record: 8-2
Simba SC is a Tanzanian football club based in Dar es Salaam. Their home games are played at two stadiums Uhuru Stadium and National Stadium. Simba SC is one of two biggest football clubs in Tanzania, their archrivals being the Young Africans. The club had several names during its history, when it was founded in 1936 it was called Queens, then changed to Eagles, Dar Sunderland and later, in 1971 changed to its actual name, Simba (that means Lion in Swahili).

Simba is the biggest also the most titled club in Tanzania.
The highest level of success that Simba SC achieved was getting to the final of the CAF Cup in 1993 where they lost to Stella Abidjan of Ivory Coast. It was the highest achievement on continental competitions reached by any Tanzanian team. One of the most memorable years for the club was 2003 when it knocked off the then reigning champions Egyptian giants Zamalek on its way to qualify for the group stages of the CAF Champions League. In the first round of that year's competition, Simba SC eliminated Santos of South Africa.
African Cup of Champions Clubs: 8 appearances
1974: Semi-Final
1976: Second Round
1977: Second Round
1978: Second Round
1979: Second Round
1980: Second Round
1981: First Round
1995: Second Round

CAF Confederation Cup: 2 appearances
2007 - Preliminary Round
2010 -
CAF Cup: 2 appearances
1993 - Finalist
1997 - First Round
CAF Cup Winners' Cup: 3 appearances
1985 - Second Round
1996 - Second Round
2001 - Second Round


Tanzanian Premier League: 17
1965, 1966 (as Sunderland)
1972, 1973, 1976, 1977, 1978, 1979, 1980, 1993, 1994, 1995, 2001, 2002, 2004, 2007, 2009/2010
Tanzanian Cup: 3
1984, 1995, 2000
Tanzanian Tusker Cup: 5
2001, 2002, 2003, 2005
2005 in Kenya
CAF Cup:
Finalist : 1993



CECAFA Clubs Cup: 6
1974, 1991, 1992, 1995, 1996, 2002
[edit] Performance in CAF competitions
CAF Champions League:
2002 - First Round
2003 - Group Stage
2004 - First Round
2005 - First Round
2008 - First Round
KOCHA Mkuu wa Taifa Stars, Jan Poulsen Pichani



amesema hapati shinikizo lolote kutokana na kauli ya aliyekuwa kocha wa timu hiyo, Mbrazili Marcio Maximo kwamba yuko tayari kurudi kufundisha Stars. Maximo alinukuliwa na gazeti hili akisema yupo tayari kurudi nchini kuifundisha Taifa Stars, kama Rais Jakaya Kikwete na Waziri Mkuu Mizengo Pinda wakimhitaji kufanya hivyo.

Akizungumza Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere, Dar es Salaam jana baada ya Stars kurejea ikitokea Morocco ilikofungwa mabao 3-1 Jumapili na kushindwa kufuzu fainali za Afrika mwakani, alisema hasumbuliwi na kauli hiyo kwani bado ana mkataba wa miaka miwili wa kuifundisha Stars. “Sina presha na alichokisema kocha huyo, zaidi ya yote bado nina mkataba wa miaka miwili wa kuifundisha timu hii na ninachoangalia ni kuiandaa timu kwa ajili ya michuano ya kufuzu fainali za Kombe la Dunia,” alisema Poulsen. Maximo alikaririwa juzi pamoja na mambo mengine akikosoa utaratibu wa sasa wa kutoinua vijana na badala yake kuita katika timu ya Taifa wachezaji wakongwe kwa sababu tu wanaishi Ughaibuni. Pia alishangaa kusikia kuwa hivi sasa Mrisho Ngassa anakalishwa benchi katika timu ya Taifa na kuingia baadaye, wakati ni mchezaji mahiri na kusema kuwa kufanya hivyo ni kuua kiwango chake. Tayari Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), limesema linasubiri ripoti ya kocha huyo ili kujua nini kifanyike kuboresha timu hiyo. Hata hivyo akizungumza jana kuhusu Stars kushindwa kufuzu fainali hizo, Poulsen alisema, wamefungwa na timu bora yenye wachezaji wengi wanaocheza Ulaya na Ligi Kuu ya England. Poulsen alisifu kiwango kilichooneshwa na timu yake kwa kudai kuwa wachezaji wake walionesha mchezo mzuri na kujituma muda wote. Akizungumzia mchezo ujao dhidi ya Chad kuwania kuingia makundi ya mchujo kwa ajili ya michezo ya kufuzu Kombe la Dunia mwaka 2014, Poulsen alisema atabadilisha kidogo kikosi hicho na kwamba wachache kati ya wachezaji waliopo sasa ndio watakaokosekana. “Nitawezaje kubadili kikosi chote? Haiwezakani, wengi watakuwepo wachache watakosekana,” alisema Poulsen.

Orijino Komedi, Jay Dee waitwa Iringa

Wasanii maarufu wa Orijino Komedi na msanii wa muziki wa kizazi kipya, Judith Wambura ‘Lady Jay Dee’ na bendi yake ya Machozi wanatarajiwa kutumika kutunisha mfuko utakaofanikisha Siku ya Utalii Duniani, ambayo kitaifa itafanyika mkoani hapa. Zaidi ya Sh milioni 120 zimekadiriwa kutumika kwa ajili ya maadhimisho ya sherehe hiyo itakayofanyika kwa wiki nzima kuanzia Septemba 28 hadi Oktoba 4, mwaka huu.



Mratibu wa Kamati ya Maandalizi ya Sherehe hizo, Fidiah Nakamendu alisema jana kwenye kikao cha maandalizi kwamba sherehe hizo zitafanyika nje kidogo ya Manispaa ya Iringa katika Kijiji cha Nduli, karibu na Uwanja wa Ndege wa Nduli. Alisema wasanii hao watafanya maonyesho yao katika mabonanza yatakayoandaliwa baadaye mjini Iringa. Alitaja mikakati mingine itakayofanikisha upatikanaji wa fedha hizo kuwa ni pamoja na kutuma barua za maombi ya michango kwa wadau mbalimbali wa utalii kama asasi za kiserikali na zisizo za kiserikali.





Mikakati mingine ni pamoja na kuandaa chakula cha hisani na kufanya tamasha la kitamaduni la chakula, mavazi na ngoma za asili. Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Mrisho ambaye ni Mwenyekiti wa sherehe hizo, ameagiza kamati hiyo ifungue akaunti maalumu ya sherehe itakayokuwa na wajumbe wawili kutoka sekta ya umma na wengine wawili kutoka sekta binafsi na kuupongeza uamuzi wa kamati kufanyia sherehe hizo karibu na Uwanja wa Ndege wa Nduli kwani utaongeza changamoto katika kuendeleza utalii wa Mkoa wa Iringa. Kulingana na waandaaji, wakati wa sherehe hizo wageni watapata fursa ya kutembelea vivutio mbalimbali vilivyopo mkoani hapa kwa gharama nafuu, pia kutakuwa na maonyesho ya vikundi mbalimbali vya burudani.

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Waziri Mkuu TUME YA KUDHIBITI UKIMWI TANZANIA

BOHARI Kuu ya Dawa nchini (MSD) imesema idadi kubwa ya dawa za kupunguza makali ya Ukimwi (ARVs) kwenye maghala yake zimekwisha muda wa matumizi na moja ya sababu ikiwa ni kuingizwa kwa dawa hizo na wafadhili bila kuzingatia mahitaji.

Mkurugenzi Mkuu wa MSD, Joseph Mgaya aliieleza Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya Ukimwi Dar es Salaam jana kuwa, Tanzania haina tatizo la dawa hizo za kurefusha maisha kwa sasa, ingawa nyingi zilizopo hazifai tena.

Akifafanua, Mgaya alisema tatizo hilo linatokea zaidi kwa ARVs za fungu la pili, zinazoletwa na wafadhili kutoka nje, maalumu kwa wagonjwa wa Ukimwi ambao virusi vinavyoshambulia kinga zao za mwili vimeshindwa kupozwa na dawa za fungu la kwanza.

“Dawa hizi tunazitegemea kutoka kwa wafadhili pekee kwa sababu Serikali haihusiki kuzinunua, zinaletwa kwetu kama msaada hasa na Mfuko wa Rais wa Marekani wa Kusaidia Mapambano dhidi ya Ukimwi (PEPRAR) kwa wagonjwa ambao virusi vinavyowashambulia ni sugu.

“Kwa kweli asilimia kubwa ya dawa hizi tulizonazo sasa zimeharibika na tumegundua sababu mbalimbali zinazochangia hali hiyo, kuwa ni pamoja na kuletwa kwa wingi bila kuzingatia mahitaji, kukosekana kwa kemikali za kupima mwendelezo wa CD4 (aina ya vitendanishi) kwa wagonjwa walioanza kutumia ARVs,” alisema Mgaya.

Sababu nyingine aliyoitaja ni kukosekana kwa fedha za kukomboa dawa hizo kutoka bandarini, mara zinapowasili kutoka nje, kutokana na utaratibu uliowekwa na Serikali unaohitaji hatua nyingi ili kupata fedha kwa ajili ya shughuli kama hiyo. Hali hiyo, alisema imesababisha dawa hizo zianze kupungua uhai wake kabla hata ya kuingia kwenye maghala hayo.

Naye Kaimu Mkurugenzi wa Ugavi wa MSD, Heri Mchunga aliiambia Kamati hiyo kuwa, pamoja na sababu hizo, kumekuwa na utaratibu usiofaa wa Serikali kubadili miongozo ya aina za dawa zinazofaa kutumika kwa wagonjwa hao, bila kuzingatia uwepo wa dawa za awali katika bohari hiyo.

Hata hivyo, Mfamasia Mkuu wa Serikali, Joseph Muhume alifafanua kwamba Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii haiwezi kubadilisha miongozo ya matumizi ya dawa ghafla, bila utaratibu na bila maelekezo ya Shirika la Afya Duniani (WHO) na kwamba, wanaofanya hivyo ni wahusika katika vituo vya afya wenyewe.

“Ni kweli kuna tatizo la wagonjwa kubadilishiwa miongozo ya dawa kiholela. Wakati wanapaswa kutumia hizo za kundi la pili, unakuta wamehamia kwenye dawa nyingine na kuzifanya zilizopo kukosa watumiaji na kuharibika, huku hali halisi ya uhitaji ikiendelea kuwepo. Serikali inalifanyia kazi suala hili,” alisema Muhume.

Alisema Serikali inatekeleza wajibu wake wa kuhakikisha kuwa dawa zote zinazoingia nchini zina asilimia 80 ya uhai, ikiwa na maana kuwa, asilimia 20 pekee ya uhai huo ndio unayoruhusiwa kisheria kupotea njiani.

Wakati huo huo, MSD imekiri kuwepo kwa tatizo la vitendanishi vinavyosaidia kugundua endapo mpimwaji ana VVU au la, na kusema tatizo hilo limechangiwa kwa kiasi kikubwa na ukosefu wa fedha za kuvinunulia huku utegemezi wa fedha kutoka kwa wafadhili ukiwakwamisha kutokana na kutozituma kwa wakati.

Mgaya alisema, mahitaji ni makubwa kuliko uwezo wao wa kununua vitendanishi hivyo kutokana na kupewa mgawo mdogo sana wa fedha kwa ajili ya ununuzi wa dawa nyingine.

“Kwa mfano katika mwaka wa fedha 2011/2012, tuliomba shilingi bilioni 158 kwa ajili ya kufanya ununuzi huo, lakini tukatengewa shilingi bilioni 78 tu. Changamoto hii ni kubwa sana katika kutekeleza mapambano dhidi ya Ukimwi na kinachokwaza zaidi ni utegemezi wetu kwa wafadhili katika kuuendeleza mradi wa Ukimwi,” alisema Mkurugenzi Mkuu wa MSD.

Hata hivyo, Muhume alijibu kuwa Serikali haina budi kuendelea kuwategemea wafadhili hao kwa sababu ni masikini na kwamba inachokitenga ndio uwezo wake, licha ya kujua ukubwa wa tatizo.

Muhume aliieleza kamati hiyo kuwa baada ya kujulishwa tatizo hilo na MSD, Serikali ilifanya jitihada na kuingiza nchini vitendanishi 34,000 vitakavyotosha kuihudumia nchi kwa miezi minne pekee, huku ikisubiri kuletewa vingine kwa ajili ya kupima CD4, vinavyotarajiwa kufika nchini mwishoni mwa mwezi huu.

“Tunafanya tuwezalo kuhakikisha kuwa hadi mwisho wa Novemba tatizo la dawa za kupima VVU linakwisha kabisa,” alisema na kuelezwa na wabunge kuwa akiwa mwakilishi wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii anapaswa kuifikishia Serikali ujumbe wa kufanya uamuzi wa kujitegemea katika vita dhidi ya Ukimwi vinginevyo wananchi wataangamia.

Wednesday, April 6, 2011

UKEKETAJI BARANI AFRICA




Mara nyingi tendo la ukeketaji unaitwa pia "tohara" kwa kulifananisha na upasuaji mdogo wa wanaume, lakini mambo ni tofauti kabisa.


Hapa sehemu za nje za viungo vya uzazi zinakatwa kusudi wasifurahie sana tendo la ndoa, hivyo wawe waaminifu zaidi kwa waume wao.

Ukeketaji umeenea hasa kati ya mataifa na makabila wenye asili ya bonde la Naili na majirani wao.

Kinyume na tohara ya wavulana matabibu wanaona hasara nyingi katika desturi hiyo. Ukeketaji unasababisha wasichana wengi kufa na wengine wengi kupatwa na maumivu makali wakati wa hedhi, wa tendo la ndoa na wa kujifungua.

Kwa sababu hizo serikali nyingi za dunia zimeupiga marufuku.

Pia madhehebu kadhaa yanatoa mafundisho kuwa ni kinyume cha masharti ya dini yao.

Mkeketaji kwa lugha ya kiswahili huiitwa “Ngariba”



Madhara ya ukeketaji
Kuhusu madhara kwa wanaokeketwa yapo mengi kwa na kuwa yamekwishatokea na kuwa malalamiko yapo mengi miongoni mwa waathirika.

“Unaweza ukakosa hamu ya kufanya ngono, au ukajifungua kwa tabu, kwa kweli madhara yapo mengi.
"na vile vile huweza kusababisha maambukizi mapya ya ugonjwa wa ukimwi kwani vifaa vinavyotumika hurudiwa kwa wasichana wengi hivyo kuweza kusababisha usambazaji wa VVU.

UUAMBUKIZO huu unaleta maumivu makali na kutoa maji maji yenye madhara makubwa, kwa sababu maji maji hayo huweza kusambaa na kuweza kuingia kwenye mfuko wa uzazi, mirija ya uzazi na hata kwenye mayai na kusababisha kuwepo kwa tatizo lisilokwisha.

Wanawake wengine huishia kuwa wagumba kwa sababu baadhi ya viungo vyao vya uzazi huharibiwa moja kwa moja, kiasi cha kutoweza kufanyiwa marekebisho tena

Wakati wa kupona baadhi ya wanawake hupata kovu lenye kitundu (keloid) na kufanya njia au uzazi kuwa ndogo.

Wapo wanawake kutokana na kukeketwa, hushindwa kushiriki vizuri tendo la ndoa kutokana na kupata maumivu na kukosa hisia, kufuatia kukatwa kwa kisimi ambacho ni sehemu muhimu kwa wanawake ili kufurahia tendo hilo.

Kwa wale wanaokeketwa au kushonwa, hali inakuwa mbaya zaidi kwa sababu mwanaume anaweza kushindwa kushiriki, kwani njia ya uke ni ndogo, hali hiyo inasababisha baadhi ya wanawake kukatwa tena ili kupanua njia.

Wanawake waliokeketwa, baadhi yao hupata shida wakati wanakwenda hedhi kwa vile njia ya uke huwa ni ndogo, hali hiyo husababisha mwanamke mwenye tatizo hili kuvimba tumbo kwa kuwa damu hushindwa kutoka nje na badala yake hujaa tumboni.

Hali hii kwa wasichana huweza kufanya wasiweze kuona damu ya hedhi na hivyo huweza kuhisiwa kuwa wana mimba na hivyo kumletea madhara.


Matatizo wakati wa ujauzito na wakati wa kujifungua hutokea mara nyingi kwa wanawake waliofanyiwa ukeketaji.


Iwapo mimba itaharibika, mabaki ya kitoto yanaweza kubaki kwenye mfuko wa uzazi na njia ya uzazi, kuwapo kovu kusababisha nyama zilizopo kwenye njia ya uzazi kushindwa kunyumbuka na kwa hali hiyo mama mjamzito kushindwa kujifungua.

Hali hiyo ya kushinda kujifungua, huweza kusababisha kifo kwa mama na mtoto aliyeko tumboni.

Mama anayejifungua anaweza kuchanika msamba ambapo sehemu ya uke na haja kubwa huungana. Uchanikaji huo humfanya mwanamke anayejifungua kupoteza damu nyingi.

Kwa kuchelewa kujifungua, mtoto anaweza kuharibika ubongo au kufa. Ili kuzuia hali hiyo isitokee, mama aliyekeketwa na kushonwa, atatakiwa kuchanwa upya ili mtoto aweze kupita bila ya matatizo.

Hata hivyo, iwapo mama huyo atajifungua nyumbani na hivyo kukosa mtu wa kumkata sehemu hiyo aliyoshonwa, atachelewa kujifungua. Basi hali kama hii itakapotokea, husababisha mama kupoteza damu nyingi, kuumia sehemu zinazozunguka eneo hilo, kupasuka msamba au uambukizo.


hivi ni baadhi ya vifaa vianvyotumika kwenye tendo la ukeketaji.
kwa kuangalia kwa macho tu utahisi kama ni vitu ambavyo havina maana machoni mwako,la hasha!!!,... Mangariba hutumia vitu kama hivyo pindi wanapoanza zoezi la ukeketaji.


ni maumizi makali wanayo pata wasichana pindi wanapokeketwa kwani hakuna hapo hakuna ganzi wala dawa ya kutuliza maumivu,hakika huu ni ukatili wa hali ya juu kwa ndugu zetu wa kiafrica kwa baadhi ya makabila.

Kwa hali hiyo juhudi za harka zinahitajika katika kuelimisha jamii juu ya suala la ukeketaji,elimu itolewe ili jamii ipate ufahamu wa mila ambazo hazina msingi na zimeshapitwa na wakati kwani ni hatari sana katika maisha ya jamii inatozunguka.
BAADHI  YA MAKABILA YANAYOFANYA UKEKETAJI
Arusha, Dodoma, Mara na Kilimanjaro na Singida, umenukuu sababu kadhaa zilizotolea kuhalalisha ukeketaji wa wanawake
Sababu hizo ni pamoja na kutunza ubikira kabla ya ndoa, kupunguza hamu ya kutaka kujamiiana na kuondoa nafasi ya kuwa na uhusiano wa mapenzi nje ya ndoa halali au mwenza kujitunza na kuondoa uwezekano wa kupata maambukizi ya ugonjwa yanayosababisha na uchafu unaojulikana kama lawalawa, kuwaongezea wanawake starehe ya tendo la ngono wakati wa kujamiiana kutokana na kutokuwapo kinembe na maji maji ukeni.

Kina mama wa makamo kiumri katika vijiji vya mikoa mitano uliofanywa utafiti huu, walisema kwamba kukeketa wanawake ni ishara ya kuonyesha kuwa msichana ametoka katika kundi la utoto na ameingia katika kundi la watu wazima, mwanamke yupo tayari kukabili ndoa.

Ni mila na desturi, sherehe za wasichana kutoka katika kundi la utoto na kujiunga na wanawake, unyago hufanywa katika jamii zisizokeketa kama vile wenyeji wa Dar-es-salaam na Pwani, kabila la Wazaramo, Wamanyema Kigoma na Wamakonde wa Mtwara

"Tujiunge kwa pamoja katika kukomesha hali hii ili kuondoa mila potofu zilizopitwa na wakati:



















Tuesday, September 7, 2010

Ujue Mkoa wa Lindi Japo kwa Ufupi



Mkoa una wilaya sita za Lindi Mjini na Lindi Vijijini, Kilwa, Nachingwea, Liwale na Ruangwa.

Mito mikubwa ndiyo Lukuledi, Matando na Mavuji, yote yaelekea Bahari Hindi. Mwinuko huanza mwambaoni ukipanda hadi mita 500, hakuna milima mirefu sana.

Wakazi

Mwaka 2002 idadi ya wakazi ilikuwa 791,306. Karibu asilimia 90 kati hao ndio wakulima. Makabila makubwa zaidi ni hasa Wamwera ambao wanapatikana hasa wilaya ya nachingwea na lindi vijijini katika kata za Rondo halafu Wamachinga ,Wamalaba ambao wako zaidi lindi mjini Wamatumbi na Wangindo huko Kilwa.

Idadi ya wakazi wa wilaya ni (idadi katika mabano): Kilwa (171,850), Lindi Mjini (41,549), Lindi Vijijini (215,764), Liwale (75,546), Nachingwea (162,081), Ruangwa (124,516),

Hali ya hewa

Hali ya hewa ya Lindi ni ya joto mwaka wote ikiwa na wastani kati ya sentigredi 24,5 na 27. Mkoa hupokea kati ya 980 mm na 1200 mm za mvua kwa mwaka, hasa kati ya miezi ya Novemba na Mei.

Miundombinu ya Mawasiliano

Kuna barabara chache katika hali nzuri. Ndizo 155 km za barabara ya lami na 3567 km barabara za udongo, mara nyingi katika hali mbaya. Wakati wa mvua mara kwa mara njia ya kwenda Daressalaam imefungwa. Kuna matumaini ya kuboreka kwa mawasiliano na mji mkuu wa Daresalaam tangu kumalizika kwa daraja la Rufiji. kwa sasa barabara ya kutoka mingoyo mpaka dar-es salaam imekamilika kwa kiwango cha lami ni kimebaki kipande cha kilometa 60 tu kuanzia Muhoro wilaya ya kilwa mpaka kukaribia daraja la Mkapa mto Rufiji ambacho kinamaliziwa kwa kiwango cha lami

Pana kiwanja cha ndege Lindi, Nachingwea na Kilwa Masoko. Lindi na Kilwa Masoko kuna pia bandari. Huduma za simu zipata maendeleo kiasi tangu kuanzishwa kwa simu za mkononi.

Utalii haujafikia umuhimu sana kutokana na matatizo ya mawasiliano magumu ingawa Lindi ina sehemu mbalimbali zenye uwezo wa kuwavuta watalii: Kilwa Kisiwani ndicho mji wa kihistoria wa pwani la Afrika ya Mashariki pamoja na magofu ya miji mingine ya Waswahili, Selous ni hifadhi kubwa kabisa katika Afrika, ufukoni wa mchanga ni wa kuvutia sana, nafasi za zamia majini ni tele.

Gesi imepatikana baharini karibu na kisiwa cha Songosongo imeleta matumaini ya maendeleo.

Kilimo na Biashara

Mkoa wa lindi wakazi wake wengi ni wakulima hasa maeneo ya vijijini wengi wanalima mazao mchanganyiko yaani ya biashara na chakula mazao ya biashara hasa ni Korosho ambazo zinapatika kwa wingi katika wilaya ya Ruangwa,Lindi Vijijini,na Nachingwea ,pia kuna zao la Ufuta na ndizi kama zao la biashara na chakula pia Mazao ya chakula kuna mahindi,mpunga,muhogo,nyanya,vitunguu hizi pia ulimwa sana wakati wa masika kutegemea na mvua za vuli. Biashara wakazi wengi wa mkoa walindi wanafanya biashara hasa biashara ndogondogo zijulikanaza kama machinga trade wanauza mazao wakati wa mavuno na uchukua bidhaa nyingi kutoka Dar-es-salaam na kupeleka vijijini hasa kwenye kata.

Elimu

mkoa wa lindi huko nyuma kielimu kwani idadi ya shule za sekondari mpaka sasa si nyingi sana na shule hizo azina walimu wa kutosha kutokana na miundombinu ya barabara na shule zenge kidato cha tano na sita mpaka sasa ni lindi sekondari-lindi,mahiwa na namupa seminari-lindi vijijini, pia kuna chuo cha uwalimu nachingwea katika wilaya ya nachingwea






WELCOME TO KUNAMBI BLOG!!!

Monday, August 16, 2010

Historia ya Tanzania kwa Ufupi.....




WELCOME TO KUNAMBI BLOG!!!

The country of Tanzania is a result of the political union between mainland Tanganyika and the off-shore islands of Zanzibar and Pemba.


* The two parts of the union attained independence from Britain separately, the mainland in 1961 and Zanzibar in 1963.

* The coastal area has been the subject of a lot of maritime rivalry first between the Portuguese and Arab traders and later between various European powers.

* It was not until the middle of the 17th century when Arab traders and slavers first entered the country.

* Zanzibar had become so important as a slaving and spice entrepot by the first half of the 18 hundreds that the Oman Sultan, Seyyid Said moved the capital there from Muscatel in 1840.

* From the beginning of the 19th century Britain's intrust stemmed when a treaty was signed with Seyyid Asides predecessor to forestall possible threats from Napoleonic France to British possessions in India.

* Seyyid Said moved to Zanzibar, the British set up their first consulate there, Britain made Oman Sultan sign treaties restricting the slave trade.

* In 1873 due to the threat of naval bombardment Sultan

Barghash (Seyyid Said's successor) signed a treaty outlawing the slave trade, although this trade continued on the mainland.

* A British protectorate was placed on Zanzibar in 1890 it remained this way until 1963 when independence was granted.

* In 1964 the Sultan was toppled in a communist-inspired revolution, during this the majority of the Arab population were massacred or expelled.

* Sultan was replaced by the Afro-Shirazi Party.

* It was during the reign of this party that Zanzibar and Pemba were merged with Tanganyika to form Tanzania.

* It was in the middle of the 19th century when the European explorers began arriving, four of the most famous being Livingstone and Stanley, Burton and Speke.

* In 1891 the Germans colonised the mainland and it was governed directly by the German government.

* The British were mandated the territory by the League of Nations after WORLD WAR 1.

* In 1954 the Tanganyika African National Union (TANU) was founded by Julius Nyerere, and they made nationalist organisations a great success.

* In 1961 Tanganyika achieved independence the country's first president was Nyerere.

* In 1967 the Arusha Declaration was created, as a result of the neglect of education, this was heavily influenced by the Chinese communist model.

* The villages were intended to be socialist organisations created by the people and governed by the people.

* Education was seen as essential to educate people into socialist ideas.

* The economy was nationalised and taxes were increased, Nyerere banned government ministers and party officials from having shares or directorships in companies or from receiving more than one salary, this was an attempt to prevent the development into an exploitative class.

* The villages since development have been transformed from peasant control to direct state control and new schemes were introduced, such as potable water, clinics, schools, fertilisers, high yield seeds and irrigation these schemes all failed due to lack of money and resentment among the peasants.

* Corruption became widespread.

* A third scheme was adopted to encourage the peasants to amalgamate their small holdings into large communially owned farms, this scheme was relatively successful and the government were prompted to adopt a policy of compulsory "villagisation" of the entire rural population.

* Nyerere turned to the People's Republic of China as his foreign partner, the Chinese built a brand new railway for Tanzania from Dar es Salaam to Kapiri Mposhi, named the TAZARA railway, due to the rise in price of oil in the 1970's Tanzania had no money to maintain the railway, there were also serious fuel shortages.

* Tanzania was bankrupted due to Nyerere's support of the guerrillas fighting for the independence of Angola and Mozambique against the Portuguese and also those fighting to overthrow the White minority government of Rhodesia.

* In 1978 Idi Amin sent his army into northern Tanzania, as a result of Tanzania supporting exiled groups who were hostile to his regime, but it was more likely that it was simply a diversion to prevent mutiny in his own country, it took months for the Tanzanians to mobilise an army but when they did face the Ugandans, the Ugandans threw down their arms and fled, the Tanzanians pushed into Uganda, they left approximately 12 000 troops within the country, Tanzania was then condemned by the OAU due to the fact that the OAU's principle is that no state should interfere with the internal affairs of another.

* Nyerere also helped to topple two other regimes in 1975 in the Comoros Islands and in 1977 in the Seychelles.

* Kenya, Tanzania and Uganda were linked together in an economic union after independence, which shared a common airline, telecommunications and postal facilities, transportations and customs, also their currencies were convertible, there was freedom of movement.

* In 1977 this fell apart as a result of political differences.

* Nyerere closed his country's borders with Kenya as a consequence of Kenya grabbing the bulk of the communities assets. These have been opened since.

* In 1985 Nyerere stepped down but he then became the chairman of his party Chana Cha Mapinduzi (the CCM-Party of the Revolution).

* Ali Hassan Mwinyi has been president since

Ngeleja: Tatizo la Lindi Mtwara ni la kiufundi

WELCOME TO KUNAMBI BLOG!!!

Ngeleja: Tatizo la Lindi Mtwara ni la kiufundi


Saturday, 29 May 2010 09:11

WAZIRI wa Nishati na Madini, William Ngeleja jana alitoa ufafanuzi wa tatizo la umeme kwenye mikoa ya Lindi na Mtwara akisema kuwa linatokana na matatizo ya kiufundi na si mvutano kati ya Shirika la Umeme (Tanesco) na kampuni binafsi ya Artumas.

Waziri Ngeleja jana aliwaambia waandishi wa habari kuwa Tanesco imepanga kuiikabidhi Artumas kazi ya kusambaza umeme kwenye mikoa hiyo ifikapo Juni mwaka huu. “Kama kuna tatizo la umeme katika mikoa hii ni technical problem (tatizo la kiufundi) na halihusiani na makabidhiano," alisema Waziri Ngeleja kwenye mkutano na waandishi wa habari.

"Kilichokwamisha makabidhiano hayo ni kutokamilika kwa ujenzi wa miundombinu katika baadhi ya maeneo. Kwa hiyo badala ya makabidhiano kufanyika mwezi Mei, sasa yatafanyika Juni.” Alisema miudombinu hiyo ni pamoja na ile inayotoka Tandahimba kwenda Masasi, pamoja na ile inayokwenda Msimbati. Alisema baada ya kukamilika kwa miundombinu hiyo, Tanesco watakabidhi jukumu la usafirishaji na usambaza umeme kwa Artumas.

Ngeleja, ambaye wizara yake inakuwa kwenye kiti moto inapofikia matatizo ya umeme, alisema katibu mkuu wa wizara hiyo yuko katika mikoa hiyo ili kuhakikisha kazi inafanyika kama ilivyopangwa. Jana vyombo vya habari viliripoti kuwa mikoa hiyo ipo katika hatari ya kukosa umeme kwa muda mrefu ujao baada ya kuibuka kwa mvutano kati ya Tanesco na Artumas kuhusu kutoa huduma hiyo. Kwa mujibu wa vyombo hivyo, mvutano huo uliibuka baada ya Artumas, iliyoingia mkataba na Tanesco Desemba mwaka 2008 wa kuzalisha, kusambaza pamoja na kutoa huduma ya umeme wa gesi katika mikoa hiyo, kushindwa kufanya hivyo.

Kwa mujibu wa ripoti hizo, mkataba huo ulitaka Artumas kupitia kampuni tanzu ya Umoja Light kuanza kutoa huduma ya umeme Machi mwaka huu, lakini ikashindwa kutokana na kudaiwa kukosa fedha, vifaa pamoja na wataalamu. Kutokana na hali hiyo, Tanesco na Umoja Light walikubaliana tena kuwa hadi kufikia Mei 30 mwaka huu, Tanesco wawe wameshaondoka katika mikoa hiyo.


Kutokana na makabaliano hayo, Tanesco ililazimika kutoa ilani ya kuwahamisha wafanyakazi wake zaidi 120 kwenda mikoa mingine. Lakini taarifa hizo zilisema Mei 21 mwaka huu watendaji wa Umoja Light waliitisha kikao cha dharura na watendaji wa Tanesco na kuomba kuongeza muda hadi Desemba mwaka huu.

Wednesday, August 11, 2010

kwa wale wote wanahitaji nafasi za kazi hebu fuata hiyo link hapo

kwa wale wenzangu naotafuta kazi hebu chungulieni kwenye http://www.tzonlinejobsearchdatabase/, kwani kuna wahitimu wengi sana wapo mitaani miaka, na bado hawajapata kazi, fuatilieni mchakato wa utangazaji wa nafasi za kazi katika link hiyo hapo juu.

WELCOME TO KUNAMBI BLOG!!!

Wednesday, August 4, 2010

Mount Kilimanjaro "The Highest Mountain in Africa" soma habari zake japo kwa ufupi hapo chini.......




Kilimanjaro. The name itself is a mystery wreathed in clouds. It might mean Mountain of Light, Mountain of Greatness or Mountain of Caravans. Or it might not. The local people, the Wachagga, don't even have a name for the whole massif, only Kipoo (now known as Kibo) for the familiar snowy peak that stands imperious, overseer of the continent, the summit of Africa.


Kilimanjaro, by any name, is a metaphor for the compelling beauty of East Africa. When you see it, you understand why. Not only is this the highest peak on the African continent; it is also the tallest free-standing mountain in the world, rising in breathtaking isolation from the surrounding coastal scrubland – elevation around 900 metres – to an imperious 5,895 metres (19,336 feet).


Kilimanjaro is one of the world's most accessible high summits, a beacon for visitors from around the world. Most climbers reach the crater rim with little more than a walking stick, proper clothing and determination. And those who reach Uhuru Point, the actual summit, or Gillman's Point on the lip of the crater, will have earned their climbing certificates and their memories.


But there is so much more to Kili than her summit. The ascent of the slopes is a virtual climatic world tour, from the tropics to the Arctic.


Even before you cross the national park boundary (at the 2,700m contour), the cultivated footslopes give way to lush montane forest, inhabited by elusive elephant, leopard, buffalo, the endangered Abbot’s duiker, and other small antelope and primates. Higher still lies the moorland zone, where a cover of giant heather is studded with otherworldly giant lobelias.

Above 4,000m, a surreal alpine desert supports little life other than a few hardy mosses and lichen. Then, finally, the last vestigial vegetation gives way to a winter wonderland of ice and snow – and the magnificent beauty of the roof of the continent.


About Kilimanjaro National Park
Size: 1668 sq km 641 sq miles).
Location: Northern Tanzania, near the town of Moshi.
Getting there
128 km (80 miles) from Arusha.
About one hour’s drive from Kilimanjaro airport.

What to do
Six usual trekking routes to the summit and other more-demanding mountaineering routes.
Day or overnight hikes on the Shira plateau. Nature trails on the lower reaches. Trout fishing.
Visit the beautiful Chala crater lake on the mountain’s southeastern slopes.
                                                                        When to go

Clearest and warmest conditions from December to February, but also dry (and colder) from July-September.

                                                                      Accommodation
Huts and campsites on the mountain. Several hotels and campsites outside the park in the village of Marangu and town of Moshi.





Fataki ni nani? Hebu fuatilia maelezo zaidi hapo chini.........

Fataki ni kampeni ya kuwakinga watoto wa kike na wanawake dhidi ya maambukizi ya virusi vya ukimwi toka kwa wanaume wanaowalaghai kwa fedha na vitu vya thamani ili kuwapata kimapenzi.





Fataki ni husika ya kufikirika aliyovikwa mwanaume mtu mzima ambaye anarubuni watoto wa kike pamoja na wanawake wengine ili kufanya nae ngono.
Fataki ni baba mtu mzima ambaye anatumia uwezo wake wa kiuchumi/kifedha kuwarubuni watu wa jinsia ya kike kutimiza lengo lake, kutokana na sifa yake hii anafikia hatua ya kubandikwa majina mengine kama ATM.
washiriki wa warsha wamechangia mawazo yao juu ya mambo muhimu ya kuzingatia katika suala zima la mawasiliano kwenye mapambano dhidi ya VVU na UKIMWI.


Washiriki hawa walianisha mambo mawili muhimu, moja likiwa ni suala la upashanaji wa habari ukizingatia tofauti za kijinsia na umri wa jamii lengwa


Jambo la pili liliowekwa bayana lilikuwa ni changamoto katika kushawishi walengwa kwenda kupima virusi vya ukimwi kwa hiari.

Washiriki walijikita katika kutengeneza mawazo na ujumbe madhubuti yanayozingatia mambo haya mawili. Baada ya kutengeneza mawazo haya walihakikisha kuwa yanafanyiwa majaribio. Majaribio haya yalifanywa mara tatu na mara zote hizi tatu walihakikisha kuwa wanayaboresha mawazo yao kutokana na maoni ya wale ambao walifanyiwa majaribio.
Washiriki waliohusishwa na mawazo na majaribio haya walikuwa ni wasanii waigizaji, watayarishaji wa vipindi vya radio, waandishi wa michezo ya kuigiza, pamoja na wachoraji wa viponzo. Kila mmoja alipewa nafasi ya kuweka mchango wake
                                            Mwisho wa warsha washiriki walifanikiwa kutoka na matangazo manne ya radio na viponzo viwili. Matangazo haya yalifanyiwa tena majaribio kwa wasikilizaji na wasomaji na hatimae kufanyiwa marekebisho kutokana na maoni katika mwezi wa September, 2008