WELCOME ALL

Gonga Hapa.

Wednesday, April 6, 2011

UKEKETAJI BARANI AFRICA




Mara nyingi tendo la ukeketaji unaitwa pia "tohara" kwa kulifananisha na upasuaji mdogo wa wanaume, lakini mambo ni tofauti kabisa.


Hapa sehemu za nje za viungo vya uzazi zinakatwa kusudi wasifurahie sana tendo la ndoa, hivyo wawe waaminifu zaidi kwa waume wao.

Ukeketaji umeenea hasa kati ya mataifa na makabila wenye asili ya bonde la Naili na majirani wao.

Kinyume na tohara ya wavulana matabibu wanaona hasara nyingi katika desturi hiyo. Ukeketaji unasababisha wasichana wengi kufa na wengine wengi kupatwa na maumivu makali wakati wa hedhi, wa tendo la ndoa na wa kujifungua.

Kwa sababu hizo serikali nyingi za dunia zimeupiga marufuku.

Pia madhehebu kadhaa yanatoa mafundisho kuwa ni kinyume cha masharti ya dini yao.

Mkeketaji kwa lugha ya kiswahili huiitwa “Ngariba”



Madhara ya ukeketaji
Kuhusu madhara kwa wanaokeketwa yapo mengi kwa na kuwa yamekwishatokea na kuwa malalamiko yapo mengi miongoni mwa waathirika.

“Unaweza ukakosa hamu ya kufanya ngono, au ukajifungua kwa tabu, kwa kweli madhara yapo mengi.
"na vile vile huweza kusababisha maambukizi mapya ya ugonjwa wa ukimwi kwani vifaa vinavyotumika hurudiwa kwa wasichana wengi hivyo kuweza kusababisha usambazaji wa VVU.

UUAMBUKIZO huu unaleta maumivu makali na kutoa maji maji yenye madhara makubwa, kwa sababu maji maji hayo huweza kusambaa na kuweza kuingia kwenye mfuko wa uzazi, mirija ya uzazi na hata kwenye mayai na kusababisha kuwepo kwa tatizo lisilokwisha.

Wanawake wengine huishia kuwa wagumba kwa sababu baadhi ya viungo vyao vya uzazi huharibiwa moja kwa moja, kiasi cha kutoweza kufanyiwa marekebisho tena

Wakati wa kupona baadhi ya wanawake hupata kovu lenye kitundu (keloid) na kufanya njia au uzazi kuwa ndogo.

Wapo wanawake kutokana na kukeketwa, hushindwa kushiriki vizuri tendo la ndoa kutokana na kupata maumivu na kukosa hisia, kufuatia kukatwa kwa kisimi ambacho ni sehemu muhimu kwa wanawake ili kufurahia tendo hilo.

Kwa wale wanaokeketwa au kushonwa, hali inakuwa mbaya zaidi kwa sababu mwanaume anaweza kushindwa kushiriki, kwani njia ya uke ni ndogo, hali hiyo inasababisha baadhi ya wanawake kukatwa tena ili kupanua njia.

Wanawake waliokeketwa, baadhi yao hupata shida wakati wanakwenda hedhi kwa vile njia ya uke huwa ni ndogo, hali hiyo husababisha mwanamke mwenye tatizo hili kuvimba tumbo kwa kuwa damu hushindwa kutoka nje na badala yake hujaa tumboni.

Hali hii kwa wasichana huweza kufanya wasiweze kuona damu ya hedhi na hivyo huweza kuhisiwa kuwa wana mimba na hivyo kumletea madhara.


Matatizo wakati wa ujauzito na wakati wa kujifungua hutokea mara nyingi kwa wanawake waliofanyiwa ukeketaji.


Iwapo mimba itaharibika, mabaki ya kitoto yanaweza kubaki kwenye mfuko wa uzazi na njia ya uzazi, kuwapo kovu kusababisha nyama zilizopo kwenye njia ya uzazi kushindwa kunyumbuka na kwa hali hiyo mama mjamzito kushindwa kujifungua.

Hali hiyo ya kushinda kujifungua, huweza kusababisha kifo kwa mama na mtoto aliyeko tumboni.

Mama anayejifungua anaweza kuchanika msamba ambapo sehemu ya uke na haja kubwa huungana. Uchanikaji huo humfanya mwanamke anayejifungua kupoteza damu nyingi.

Kwa kuchelewa kujifungua, mtoto anaweza kuharibika ubongo au kufa. Ili kuzuia hali hiyo isitokee, mama aliyekeketwa na kushonwa, atatakiwa kuchanwa upya ili mtoto aweze kupita bila ya matatizo.

Hata hivyo, iwapo mama huyo atajifungua nyumbani na hivyo kukosa mtu wa kumkata sehemu hiyo aliyoshonwa, atachelewa kujifungua. Basi hali kama hii itakapotokea, husababisha mama kupoteza damu nyingi, kuumia sehemu zinazozunguka eneo hilo, kupasuka msamba au uambukizo.


hivi ni baadhi ya vifaa vianvyotumika kwenye tendo la ukeketaji.
kwa kuangalia kwa macho tu utahisi kama ni vitu ambavyo havina maana machoni mwako,la hasha!!!,... Mangariba hutumia vitu kama hivyo pindi wanapoanza zoezi la ukeketaji.


ni maumizi makali wanayo pata wasichana pindi wanapokeketwa kwani hakuna hapo hakuna ganzi wala dawa ya kutuliza maumivu,hakika huu ni ukatili wa hali ya juu kwa ndugu zetu wa kiafrica kwa baadhi ya makabila.

Kwa hali hiyo juhudi za harka zinahitajika katika kuelimisha jamii juu ya suala la ukeketaji,elimu itolewe ili jamii ipate ufahamu wa mila ambazo hazina msingi na zimeshapitwa na wakati kwani ni hatari sana katika maisha ya jamii inatozunguka.
BAADHI  YA MAKABILA YANAYOFANYA UKEKETAJI
Arusha, Dodoma, Mara na Kilimanjaro na Singida, umenukuu sababu kadhaa zilizotolea kuhalalisha ukeketaji wa wanawake
Sababu hizo ni pamoja na kutunza ubikira kabla ya ndoa, kupunguza hamu ya kutaka kujamiiana na kuondoa nafasi ya kuwa na uhusiano wa mapenzi nje ya ndoa halali au mwenza kujitunza na kuondoa uwezekano wa kupata maambukizi ya ugonjwa yanayosababisha na uchafu unaojulikana kama lawalawa, kuwaongezea wanawake starehe ya tendo la ngono wakati wa kujamiiana kutokana na kutokuwapo kinembe na maji maji ukeni.

Kina mama wa makamo kiumri katika vijiji vya mikoa mitano uliofanywa utafiti huu, walisema kwamba kukeketa wanawake ni ishara ya kuonyesha kuwa msichana ametoka katika kundi la utoto na ameingia katika kundi la watu wazima, mwanamke yupo tayari kukabili ndoa.

Ni mila na desturi, sherehe za wasichana kutoka katika kundi la utoto na kujiunga na wanawake, unyago hufanywa katika jamii zisizokeketa kama vile wenyeji wa Dar-es-salaam na Pwani, kabila la Wazaramo, Wamanyema Kigoma na Wamakonde wa Mtwara

"Tujiunge kwa pamoja katika kukomesha hali hii ili kuondoa mila potofu zilizopitwa na wakati:



















Tuesday, September 7, 2010

Ujue Mkoa wa Lindi Japo kwa Ufupi



Mkoa una wilaya sita za Lindi Mjini na Lindi Vijijini, Kilwa, Nachingwea, Liwale na Ruangwa.

Mito mikubwa ndiyo Lukuledi, Matando na Mavuji, yote yaelekea Bahari Hindi. Mwinuko huanza mwambaoni ukipanda hadi mita 500, hakuna milima mirefu sana.

Wakazi

Mwaka 2002 idadi ya wakazi ilikuwa 791,306. Karibu asilimia 90 kati hao ndio wakulima. Makabila makubwa zaidi ni hasa Wamwera ambao wanapatikana hasa wilaya ya nachingwea na lindi vijijini katika kata za Rondo halafu Wamachinga ,Wamalaba ambao wako zaidi lindi mjini Wamatumbi na Wangindo huko Kilwa.

Idadi ya wakazi wa wilaya ni (idadi katika mabano): Kilwa (171,850), Lindi Mjini (41,549), Lindi Vijijini (215,764), Liwale (75,546), Nachingwea (162,081), Ruangwa (124,516),

Hali ya hewa

Hali ya hewa ya Lindi ni ya joto mwaka wote ikiwa na wastani kati ya sentigredi 24,5 na 27. Mkoa hupokea kati ya 980 mm na 1200 mm za mvua kwa mwaka, hasa kati ya miezi ya Novemba na Mei.

Miundombinu ya Mawasiliano

Kuna barabara chache katika hali nzuri. Ndizo 155 km za barabara ya lami na 3567 km barabara za udongo, mara nyingi katika hali mbaya. Wakati wa mvua mara kwa mara njia ya kwenda Daressalaam imefungwa. Kuna matumaini ya kuboreka kwa mawasiliano na mji mkuu wa Daresalaam tangu kumalizika kwa daraja la Rufiji. kwa sasa barabara ya kutoka mingoyo mpaka dar-es salaam imekamilika kwa kiwango cha lami ni kimebaki kipande cha kilometa 60 tu kuanzia Muhoro wilaya ya kilwa mpaka kukaribia daraja la Mkapa mto Rufiji ambacho kinamaliziwa kwa kiwango cha lami

Pana kiwanja cha ndege Lindi, Nachingwea na Kilwa Masoko. Lindi na Kilwa Masoko kuna pia bandari. Huduma za simu zipata maendeleo kiasi tangu kuanzishwa kwa simu za mkononi.

Utalii haujafikia umuhimu sana kutokana na matatizo ya mawasiliano magumu ingawa Lindi ina sehemu mbalimbali zenye uwezo wa kuwavuta watalii: Kilwa Kisiwani ndicho mji wa kihistoria wa pwani la Afrika ya Mashariki pamoja na magofu ya miji mingine ya Waswahili, Selous ni hifadhi kubwa kabisa katika Afrika, ufukoni wa mchanga ni wa kuvutia sana, nafasi za zamia majini ni tele.

Gesi imepatikana baharini karibu na kisiwa cha Songosongo imeleta matumaini ya maendeleo.

Kilimo na Biashara

Mkoa wa lindi wakazi wake wengi ni wakulima hasa maeneo ya vijijini wengi wanalima mazao mchanganyiko yaani ya biashara na chakula mazao ya biashara hasa ni Korosho ambazo zinapatika kwa wingi katika wilaya ya Ruangwa,Lindi Vijijini,na Nachingwea ,pia kuna zao la Ufuta na ndizi kama zao la biashara na chakula pia Mazao ya chakula kuna mahindi,mpunga,muhogo,nyanya,vitunguu hizi pia ulimwa sana wakati wa masika kutegemea na mvua za vuli. Biashara wakazi wengi wa mkoa walindi wanafanya biashara hasa biashara ndogondogo zijulikanaza kama machinga trade wanauza mazao wakati wa mavuno na uchukua bidhaa nyingi kutoka Dar-es-salaam na kupeleka vijijini hasa kwenye kata.

Elimu

mkoa wa lindi huko nyuma kielimu kwani idadi ya shule za sekondari mpaka sasa si nyingi sana na shule hizo azina walimu wa kutosha kutokana na miundombinu ya barabara na shule zenge kidato cha tano na sita mpaka sasa ni lindi sekondari-lindi,mahiwa na namupa seminari-lindi vijijini, pia kuna chuo cha uwalimu nachingwea katika wilaya ya nachingwea






WELCOME TO KUNAMBI BLOG!!!

Monday, August 16, 2010

Historia ya Tanzania kwa Ufupi.....




WELCOME TO KUNAMBI BLOG!!!

The country of Tanzania is a result of the political union between mainland Tanganyika and the off-shore islands of Zanzibar and Pemba.


* The two parts of the union attained independence from Britain separately, the mainland in 1961 and Zanzibar in 1963.

* The coastal area has been the subject of a lot of maritime rivalry first between the Portuguese and Arab traders and later between various European powers.

* It was not until the middle of the 17th century when Arab traders and slavers first entered the country.

* Zanzibar had become so important as a slaving and spice entrepot by the first half of the 18 hundreds that the Oman Sultan, Seyyid Said moved the capital there from Muscatel in 1840.

* From the beginning of the 19th century Britain's intrust stemmed when a treaty was signed with Seyyid Asides predecessor to forestall possible threats from Napoleonic France to British possessions in India.

* Seyyid Said moved to Zanzibar, the British set up their first consulate there, Britain made Oman Sultan sign treaties restricting the slave trade.

* In 1873 due to the threat of naval bombardment Sultan

Barghash (Seyyid Said's successor) signed a treaty outlawing the slave trade, although this trade continued on the mainland.

* A British protectorate was placed on Zanzibar in 1890 it remained this way until 1963 when independence was granted.

* In 1964 the Sultan was toppled in a communist-inspired revolution, during this the majority of the Arab population were massacred or expelled.

* Sultan was replaced by the Afro-Shirazi Party.

* It was during the reign of this party that Zanzibar and Pemba were merged with Tanganyika to form Tanzania.

* It was in the middle of the 19th century when the European explorers began arriving, four of the most famous being Livingstone and Stanley, Burton and Speke.

* In 1891 the Germans colonised the mainland and it was governed directly by the German government.

* The British were mandated the territory by the League of Nations after WORLD WAR 1.

* In 1954 the Tanganyika African National Union (TANU) was founded by Julius Nyerere, and they made nationalist organisations a great success.

* In 1961 Tanganyika achieved independence the country's first president was Nyerere.

* In 1967 the Arusha Declaration was created, as a result of the neglect of education, this was heavily influenced by the Chinese communist model.

* The villages were intended to be socialist organisations created by the people and governed by the people.

* Education was seen as essential to educate people into socialist ideas.

* The economy was nationalised and taxes were increased, Nyerere banned government ministers and party officials from having shares or directorships in companies or from receiving more than one salary, this was an attempt to prevent the development into an exploitative class.

* The villages since development have been transformed from peasant control to direct state control and new schemes were introduced, such as potable water, clinics, schools, fertilisers, high yield seeds and irrigation these schemes all failed due to lack of money and resentment among the peasants.

* Corruption became widespread.

* A third scheme was adopted to encourage the peasants to amalgamate their small holdings into large communially owned farms, this scheme was relatively successful and the government were prompted to adopt a policy of compulsory "villagisation" of the entire rural population.

* Nyerere turned to the People's Republic of China as his foreign partner, the Chinese built a brand new railway for Tanzania from Dar es Salaam to Kapiri Mposhi, named the TAZARA railway, due to the rise in price of oil in the 1970's Tanzania had no money to maintain the railway, there were also serious fuel shortages.

* Tanzania was bankrupted due to Nyerere's support of the guerrillas fighting for the independence of Angola and Mozambique against the Portuguese and also those fighting to overthrow the White minority government of Rhodesia.

* In 1978 Idi Amin sent his army into northern Tanzania, as a result of Tanzania supporting exiled groups who were hostile to his regime, but it was more likely that it was simply a diversion to prevent mutiny in his own country, it took months for the Tanzanians to mobilise an army but when they did face the Ugandans, the Ugandans threw down their arms and fled, the Tanzanians pushed into Uganda, they left approximately 12 000 troops within the country, Tanzania was then condemned by the OAU due to the fact that the OAU's principle is that no state should interfere with the internal affairs of another.

* Nyerere also helped to topple two other regimes in 1975 in the Comoros Islands and in 1977 in the Seychelles.

* Kenya, Tanzania and Uganda were linked together in an economic union after independence, which shared a common airline, telecommunications and postal facilities, transportations and customs, also their currencies were convertible, there was freedom of movement.

* In 1977 this fell apart as a result of political differences.

* Nyerere closed his country's borders with Kenya as a consequence of Kenya grabbing the bulk of the communities assets. These have been opened since.

* In 1985 Nyerere stepped down but he then became the chairman of his party Chana Cha Mapinduzi (the CCM-Party of the Revolution).

* Ali Hassan Mwinyi has been president since

Ngeleja: Tatizo la Lindi Mtwara ni la kiufundi

WELCOME TO KUNAMBI BLOG!!!

Ngeleja: Tatizo la Lindi Mtwara ni la kiufundi


Saturday, 29 May 2010 09:11

WAZIRI wa Nishati na Madini, William Ngeleja jana alitoa ufafanuzi wa tatizo la umeme kwenye mikoa ya Lindi na Mtwara akisema kuwa linatokana na matatizo ya kiufundi na si mvutano kati ya Shirika la Umeme (Tanesco) na kampuni binafsi ya Artumas.

Waziri Ngeleja jana aliwaambia waandishi wa habari kuwa Tanesco imepanga kuiikabidhi Artumas kazi ya kusambaza umeme kwenye mikoa hiyo ifikapo Juni mwaka huu. “Kama kuna tatizo la umeme katika mikoa hii ni technical problem (tatizo la kiufundi) na halihusiani na makabidhiano," alisema Waziri Ngeleja kwenye mkutano na waandishi wa habari.

"Kilichokwamisha makabidhiano hayo ni kutokamilika kwa ujenzi wa miundombinu katika baadhi ya maeneo. Kwa hiyo badala ya makabidhiano kufanyika mwezi Mei, sasa yatafanyika Juni.” Alisema miudombinu hiyo ni pamoja na ile inayotoka Tandahimba kwenda Masasi, pamoja na ile inayokwenda Msimbati. Alisema baada ya kukamilika kwa miundombinu hiyo, Tanesco watakabidhi jukumu la usafirishaji na usambaza umeme kwa Artumas.

Ngeleja, ambaye wizara yake inakuwa kwenye kiti moto inapofikia matatizo ya umeme, alisema katibu mkuu wa wizara hiyo yuko katika mikoa hiyo ili kuhakikisha kazi inafanyika kama ilivyopangwa. Jana vyombo vya habari viliripoti kuwa mikoa hiyo ipo katika hatari ya kukosa umeme kwa muda mrefu ujao baada ya kuibuka kwa mvutano kati ya Tanesco na Artumas kuhusu kutoa huduma hiyo. Kwa mujibu wa vyombo hivyo, mvutano huo uliibuka baada ya Artumas, iliyoingia mkataba na Tanesco Desemba mwaka 2008 wa kuzalisha, kusambaza pamoja na kutoa huduma ya umeme wa gesi katika mikoa hiyo, kushindwa kufanya hivyo.

Kwa mujibu wa ripoti hizo, mkataba huo ulitaka Artumas kupitia kampuni tanzu ya Umoja Light kuanza kutoa huduma ya umeme Machi mwaka huu, lakini ikashindwa kutokana na kudaiwa kukosa fedha, vifaa pamoja na wataalamu. Kutokana na hali hiyo, Tanesco na Umoja Light walikubaliana tena kuwa hadi kufikia Mei 30 mwaka huu, Tanesco wawe wameshaondoka katika mikoa hiyo.


Kutokana na makabaliano hayo, Tanesco ililazimika kutoa ilani ya kuwahamisha wafanyakazi wake zaidi 120 kwenda mikoa mingine. Lakini taarifa hizo zilisema Mei 21 mwaka huu watendaji wa Umoja Light waliitisha kikao cha dharura na watendaji wa Tanesco na kuomba kuongeza muda hadi Desemba mwaka huu.

Wednesday, August 11, 2010

kwa wale wote wanahitaji nafasi za kazi hebu fuata hiyo link hapo

kwa wale wenzangu naotafuta kazi hebu chungulieni kwenye http://www.tzonlinejobsearchdatabase/, kwani kuna wahitimu wengi sana wapo mitaani miaka, na bado hawajapata kazi, fuatilieni mchakato wa utangazaji wa nafasi za kazi katika link hiyo hapo juu.

WELCOME TO KUNAMBI BLOG!!!

Wednesday, August 4, 2010

Mount Kilimanjaro "The Highest Mountain in Africa" soma habari zake japo kwa ufupi hapo chini.......




Kilimanjaro. The name itself is a mystery wreathed in clouds. It might mean Mountain of Light, Mountain of Greatness or Mountain of Caravans. Or it might not. The local people, the Wachagga, don't even have a name for the whole massif, only Kipoo (now known as Kibo) for the familiar snowy peak that stands imperious, overseer of the continent, the summit of Africa.


Kilimanjaro, by any name, is a metaphor for the compelling beauty of East Africa. When you see it, you understand why. Not only is this the highest peak on the African continent; it is also the tallest free-standing mountain in the world, rising in breathtaking isolation from the surrounding coastal scrubland – elevation around 900 metres – to an imperious 5,895 metres (19,336 feet).


Kilimanjaro is one of the world's most accessible high summits, a beacon for visitors from around the world. Most climbers reach the crater rim with little more than a walking stick, proper clothing and determination. And those who reach Uhuru Point, the actual summit, or Gillman's Point on the lip of the crater, will have earned their climbing certificates and their memories.


But there is so much more to Kili than her summit. The ascent of the slopes is a virtual climatic world tour, from the tropics to the Arctic.


Even before you cross the national park boundary (at the 2,700m contour), the cultivated footslopes give way to lush montane forest, inhabited by elusive elephant, leopard, buffalo, the endangered Abbot’s duiker, and other small antelope and primates. Higher still lies the moorland zone, where a cover of giant heather is studded with otherworldly giant lobelias.

Above 4,000m, a surreal alpine desert supports little life other than a few hardy mosses and lichen. Then, finally, the last vestigial vegetation gives way to a winter wonderland of ice and snow – and the magnificent beauty of the roof of the continent.


About Kilimanjaro National Park
Size: 1668 sq km 641 sq miles).
Location: Northern Tanzania, near the town of Moshi.
Getting there
128 km (80 miles) from Arusha.
About one hour’s drive from Kilimanjaro airport.

What to do
Six usual trekking routes to the summit and other more-demanding mountaineering routes.
Day or overnight hikes on the Shira plateau. Nature trails on the lower reaches. Trout fishing.
Visit the beautiful Chala crater lake on the mountain’s southeastern slopes.
                                                                        When to go

Clearest and warmest conditions from December to February, but also dry (and colder) from July-September.

                                                                      Accommodation
Huts and campsites on the mountain. Several hotels and campsites outside the park in the village of Marangu and town of Moshi.





Fataki ni nani? Hebu fuatilia maelezo zaidi hapo chini.........

Fataki ni kampeni ya kuwakinga watoto wa kike na wanawake dhidi ya maambukizi ya virusi vya ukimwi toka kwa wanaume wanaowalaghai kwa fedha na vitu vya thamani ili kuwapata kimapenzi.





Fataki ni husika ya kufikirika aliyovikwa mwanaume mtu mzima ambaye anarubuni watoto wa kike pamoja na wanawake wengine ili kufanya nae ngono.
Fataki ni baba mtu mzima ambaye anatumia uwezo wake wa kiuchumi/kifedha kuwarubuni watu wa jinsia ya kike kutimiza lengo lake, kutokana na sifa yake hii anafikia hatua ya kubandikwa majina mengine kama ATM.
washiriki wa warsha wamechangia mawazo yao juu ya mambo muhimu ya kuzingatia katika suala zima la mawasiliano kwenye mapambano dhidi ya VVU na UKIMWI.


Washiriki hawa walianisha mambo mawili muhimu, moja likiwa ni suala la upashanaji wa habari ukizingatia tofauti za kijinsia na umri wa jamii lengwa


Jambo la pili liliowekwa bayana lilikuwa ni changamoto katika kushawishi walengwa kwenda kupima virusi vya ukimwi kwa hiari.

Washiriki walijikita katika kutengeneza mawazo na ujumbe madhubuti yanayozingatia mambo haya mawili. Baada ya kutengeneza mawazo haya walihakikisha kuwa yanafanyiwa majaribio. Majaribio haya yalifanywa mara tatu na mara zote hizi tatu walihakikisha kuwa wanayaboresha mawazo yao kutokana na maoni ya wale ambao walifanyiwa majaribio.
Washiriki waliohusishwa na mawazo na majaribio haya walikuwa ni wasanii waigizaji, watayarishaji wa vipindi vya radio, waandishi wa michezo ya kuigiza, pamoja na wachoraji wa viponzo. Kila mmoja alipewa nafasi ya kuweka mchango wake
                                            Mwisho wa warsha washiriki walifanikiwa kutoka na matangazo manne ya radio na viponzo viwili. Matangazo haya yalifanyiwa tena majaribio kwa wasikilizaji na wasomaji na hatimae kufanyiwa marekebisho kutokana na maoni katika mwezi wa September, 2008

Tuesday, August 3, 2010

Je unalijua Kabila lako? Haya ni Makabila Yanayopatikana Nchini Tanzania


Hii Ni Orodha Ya Makabila Ya Tanzania.
Kuna matatizo kwenye majina kadhaa katika orodha hii, kwasababu mbalimbali. Orodha hii inatokana na orodha ya Ethnologue ya lugha za Tanzania, pamoja na tovuti nyingine. Inawezekana kwamba baadhi ya majina ya makabila ni majina ya lugha au lahaja badala ya makabila, na labda majina mengine yaliandikwa vibaya. Juu ya hivyo, hakuna ufafanuzi wa wazi kusema kwamba kikundi fulani ni kabila au siyo. Vikundi kadhaa katika orodha hii vina wenyeji mamia tu, lakini vikundi vingine vinavyo mamilioni ya watu; labda kila kikundi kinaitwa "kabila," lakini ni jamii za aina tofauti kabisa. Vikundi katika ukurasa huu vimeorodheshwa kuwa vikundi tofauti kutokana na ushahidi kutoka Ethnologue kutofautisha lugha zao.

Hii ni orodha ya makabila ya watu ambao wamekuwa wanaishi tangu zamani katika eneo ambalo sasa linaitwa Tanzania, pamoja na makabila yaliyogawiwa na mipaka baina ya Tanzania na nchi za jirani. Orodha hii haizingatii makabila yanayoishi katika Tanzania kama wakimbizi kutoka vita katika nchi za jirani. Ukurasa huu hauorodheshi vikundi vya wahamiaji kutoka nchi za kigeni, kama wahamiaji au wazao wao kutoka Arabia au Uhindi.

Waalagwa (pia wanaitwa Wasi),wanatokea Mkoa wa Dodoma, Wilaya ya Kondoa. Lugha yao ni Chasi. Waakiek,Waarusha,Waassa,

 Wabembe ni kabila la Tanzania wanaoishi katika Mkoa wa Kigoma, Wilaya ya Kigoma Vijijini. Lugha yao ni Kibembe.

, Wabena ni kabila la watu wa Tanzania wanaoishi hasa katika Mkoa wa Iringa, Wilaya ya Njombe.Lugha yao ni Kibena

, Wabende ni kabila la Tanzania wanaoishi katika Mkoa wa Rukwa, Wilaya ya Mpanda. Lugha yao ni Kibende,

Wabondei ni kabila la Tanzania wanaoishi katika Mkoa wa Tanga, karibu na Milima ya Usambara. Lugha yao ni Kibondei.

, Wabungu ni kabila la Tanzania wanaoishi katika Mkoa wa Mbeya, Wilaya ya Chunya. Lugha yao ni Kibungu.

Waburunge ni kabila la Tanzania wanaoishi katika Mkoa wa Dodoma, Wilaya ya Kondoa. Lugha yao ni Kiburunge

, Wachagga ni kabila la watu wenye asili ya Kibantu wanaoishi kaskazini mwa Tanzania chini ya mlima Kilimanjaro, mkoani Kilimanjaro. Shughuli kubwa ya Wachagga ni biashara na kilimo. Wachagga wana historia ndefu ya asili yao na maingiliano yao na makabila mengine. Kabila la kichagga ni mkusanyiko wa makabila madogo madogo (ya Kichagga) yaliyosambaa kijiografia kuzunguka mlima Kilimanjaro kuanzia Mashariki Tarakea, Rombo hadi magharibi ya Kilimanjaro Siha, Machame. Makabila ya Kichagga ni Wa-Rombo, Wa-Marangu, Wa-Old Moshi, Wa-Kibosho, na Wa-Machame. Makundi mengine madogo ya wachagga ni Wakirua-Vunjo, Wa-Uru, na Wa-Siha.

• Lugha ya Kichagga, inabadilika kuanzia unapotoka Tarakea mpaka unapofika Siha magharibi mwa Kilimanjaro. Kutokana na tofauti hizo Kichagga kimegawanyika katika Kirombo, Kimarangu, Ki-Old Moshi,Kikibosho, Kimachame, Kikirua na Kisiha. Lugha hizi zinakaribia kufanana kulingana na jinsi makabila hayo yalivyopakana. Kwa mfano, Ki-Old Moshi kinafanana na Kikirua, ambacho nacho kinafanana kidogo na Kimarangu. Vile vile Kisiha kinafanana sana na Kimachame ambacho pia kinafanana kidogo na Kikibosho. Baadhi ya Wamachame walihamia sehemu za Meru Arusha na kuchanganyikana na Waarusha, lugha yao ikabadilika kidogo na kuwa Ki-meru. Kwa sababu hii Wameru wanasikilizana sana na Wamachame ingawa lafudhi zao zinatofautiana kidogo.

Majina ya Kichagga

Majina ya kiukoo ya Kichagga pia huashiria wanatoka sehemu gani ya Uchaga, japo si lazima kuwa hivyo: mfano familia maarufu za Kichagga nchini Tanzania ni kama Kimaro, Swai, Massawe, Mushi, Lema, Urassa, Nkya, Ndosi, Meena hutoka Machame. Akina Temu, Mlaki, Mlay, Lyimo, Moshiro, Mselle, Kileo, Kimambo, Tesha wanatoka Old Moshi na Vunjo. Mariki, Tarimo, Laswai, Mallya, Mrema, Mkenda, Massawe, Lamtey, Tairo, Mramba, Kauki wanatoka Rombo. Sawe, Usiri, Shayo, Kiwelu, Makundi, Urasa, Moshi, Meela, Minja, Njau wanatoka Marangu. Rite, Makule, Minja, Mashayo, Chao, Shao, Makawia, Ndesano, Kimario, Tilla, Mariale, Tarimo, Mafole, Kituo, Mrosso, Lyakundia, Kessy, Mmbando, Matemba, Ndenshau, Morio, Akaro, Matowo, Towo, Mkony, Temba na kadhalika hutoka Kibosho.

Wachagga wengi hupenda kurudi nyumbani kipindi cha Krismasi, ikiwa ni kuwatembelea wazazi wao, rafiki, au ndugu. Ingawa wengi hudhani kwamba Wachagga wameathiriwa sana na dini ya Ukristo kwa kuwa wengi wao ni Wakristo na hiki huwa ni kipindi cha likizo kwao, inaaminika pia kuwa kurudi kwao Uchagani wakati wa Krismasi ni pamoja na kutembelea ndugu zao na kujumuika pamoja katika kuumaliza mwaka baada ya kazi nyingi za kutafuta pesa kwa mwaka mzima.

Wadatooga (pia huitwa Wataturu, Wamang'ati au Wabarabaig) ni kabila la Tanzania wanaoishi katika mikoa ya Manyara na Singida. Lugha yao ni Kidatooga

Wadigo ni kabila la Tanzania wanaoishi katika Mkoa wa Tanga, hasa kwenye mji wa Tanga. Pia wako Kenya wanapoishi upande wa Kusini wa mji wa Mombasa. Katika Kenya huhesabiwa kati ya mijikenda. Lugha yao ni Kidigo.

, Wadoe ni kabila la Tanzania wanaoishi katika Mkoa wa Pwani, Wilaya ya Bagamoyo. Lugha yao ni Kidoe.

, Wafipa ni kabila la Tanzania wanaoishi katika Mkoa wa Rukwa, hasa katika wilaya za Sumbawanga na Nkansi. Lugha yao ni Kifipa.

, Wagogo (mmojawao anaitwa Mgogo) ni kabila la Tanzania ya kati, wenyeji wa mikoa ya Dodoma na Singida. Lugha yao ni Cigogo (kwa Kiswahili hutamkika Kigogo).

Dini ya wengi wao ni Ukristo, hasa wa madhehebu ya Anglikana, halafu wa Kanisa Katoliki. Historia ya Wagogo inaweza kuelezeka kwa kuangalia yafuatayo: Utawala wa jadi, nyumba za asili, chakula kikuu na lafudhi ya lugha. Majina ya ukoo ya Cigogo

majina hayo ni kama Mazengo, Cidosa, Cilongani, Malecela, Mwaluko, Mavunde, Ndejembi, Manyesela, Mbogambi, Mdachi, Kapaya,Matonya, Mtunya, Kusila, Nhonya,Mhalanyuka, Mbenaa, Chibile, Mdoli, Lusinde,Njamasi,Majenda,Chiwamba,Mazoya,Ufinyu,Chilyawanhu,Magaya, Ngoli,Chiwanga,Lubeleje,Makupila,Fukunyi

Waha ni kabila la Tanzania wanaoishi katika Mkoa wa Kigoma, pia mpakani na Burundi. Lugha yao ni Kiha.

Wahaya ni Kabila linalopatikana katika Mkoa wa Kagera, Kaskazini Magharibi mwa Tanzania, kandokando mwa Ziwa Victoria. Lugha yao ni Kihaya

Wahehe ni kabila la Tanzania ambalo kiasili linaishi katika wilaya za kaskazini za Mkoa wa Iringa, yaani Iringa, Kilolo na Mafinga.

Ni moja kati ya makabila yaliyotokea kwenye bonde la mto Rufiji. Ndiyo sababu wanazika wafu wao wakielekea mashariki.

Lugha yao (Kihehe) imegawanyika kiasi fulani katika lahaja (matamshi) tofautitofauti kutokana na maeneo ambayo huzungumzwa. Inafanana kimatamshi na kimaana na lugha ya Kibena iliyopo wilayani Njombe.

Wajita ni kabila la Tanzania wanaoishi katika Mkoa wa Mara. Lugha yao ni Kijita.

Wakaguru ni kabila la Tanzania wanaoishi katika Mkoa wa Morogoro, Wilaya ya Kilosa. Lugha yao ni Kikaguru.

Wakinga ni kabila la Tanzania wanaoishi katika Mkoa wa Iringa, Wilaya ya Makete. Lugha yao ni Kikinga

Wakuria ni kabila la Tanzania wanaoishi katika Mkoa wa Mara, pia wako Kenya. Lugha yao ni Kikuria


Waluguru ni kabila la Tanzania wanaoishi katika mikoa ya Morogoro na Pwani, hasa kwenye Milima ya Uluguru. Lugha yao ni Kiluguru.


Waluo (pia Wajaluo) ni kabila hasa la Kenya. Wako pia Uganda ya msahriki na wachache wanaishi nchini Tanzania katika Mkoa wa Mara. Lugha yao ni Kiluo. Wenyewe hujiita Jaluo na lugha yao Dhulou.na mengi kuhusu waluo.tembelea websitehii;www.jaluo.com utacheka mpaka ujambe puuu.ongito nyamwanda 0784334032 en an jakiseru jakanyango

Waluo ni mkusanyiko wa kabila la kinilotiki ambalo lilisafiri kutoka Afrika ya Kaskazini kufuata mto Nile kuja Kusini. Waluo wengi wameenea kandokando ya Ziwa Viktoria kutokana na utamaduni wao wa uvuvi. Kwa Afrika mashariki utawakuta nchini Sudan, Kenya, Uganda na Tanzania.Waluo mashuhuri

• Gidi Gidi Maji Maji - Waimbaji wa hiphop

• Tom Mboya - mwanasiasa aliyeuawa 1969

• Barack Obama - mwanasiasa na seneta wa Marekani ni mwana wa baba Mluo

• Jaramogi Oginga Odinga - kiongozi wa Waluo wakati wa uhuru, mwanzilishaji wa chama cha KANU na makamu wa rais wa kwanza

• Raila Amolo Odinga - mwana wa Jaramogi na mwanasiasa muhimu wa kitaifa

• Robert Ouko - waziri wa mambo ya nje aliyeuawa 1990

Wamasai ni kabila wazawa wa Afrika la watu wahamaji katika wanaopatikana Kenya kaskazini Tanzania.


Wamachinga ni kabila la Tanzania wanaoishi katika Mkoa wa Lindi, wilaya za Kilwa na Lindi. Lugha yao ni Kimachinga.

Kwa kipindi cha karne ya 21 wamekuwa maarufu katika miji kwa kuuza bidhaa wakiwa wameshika mkononi wakisaka wateja.

Wamakonde ni kabila la Tanzania wanaoishi katika Mkoa wa Mtwara. Pia wako Msumbiji. Lugha yao ni Kimakonde.

Wamwera ni kabila la Tanzania wanaoishi katika Mkoa wa Lindi, hasa kwenye Wilaya ya Nachingwea. Lugha yao ni Kimwera.

Wandengereko ni kabila la Tanzania wanaoishi katika Mkoa wa Pwani, Wilaya ya Rufiji. Lugha yao ni Kindengereko.Hapana, Wandengereko hawaishi Mkoa wa Ruvuma bali mkoa wa Pwani kusini ya Dar es salaam katika Wilaya za Mkuranga na Rufiji.

Wangindo ni kabila la Tanzania wanaoishi upande wa Kusini wa Tanzania. Lugha yao ni Kingindo,

Wanyakyusa (pia huitwa Wangonde au Wasochile) ni jina kwa ajili ya watu wanaoishi kwenye wilaya ya Rungwe katika sehemu za kusini za Mkoa wa Mbeya (Tanzania) upande wa kaskazini ya Ziwa Nyasa. Lugha yao ni Kinyakyusa. Mara nyingi Wagonde upande wa kusini ya mto Songwe nchini Malawi huhesabiwa pamoja nao katika kundi lilelile.

Kihistoria watu wanaoitwa leo Wanyakyusa waliitwa Wakonde na Wanyakyusa walikuwa kabila kubwa kati yao. Wakati wa karne ya 20 "Wanyakyusa" imekuwa jina la kundi kwa jumla. Hadi leo kanisa la kilutheri la KKKT linatumia jina "dayosisi ya Konde" kwa eneo lake katika mkoa wa Mbeya.

Wakati Wajerumani walipofika sehemu za kaskazini ya Ziwa Nyasa mwisho wa karne ya 19 hawakuona tofauti ya kimsingi kati ya watu wa Malawi kaskazini na wale wa sehemu za Rungwe wakawaita wote "Wakonde" kutokana na jina lililokuwa kawaida ziwani.

Leo hii ni watu zaidi ya milioni wanaojumlishwa kwa jina hili, takriban 700,000 wanaokaa upande wa Tanzania na 300,000 wakikaa Malawi.

Wanyamwezi ni kabila la Tanzania wanaoishi katika mikoa ya Tabora na Shinyanga. Lugha yao ni Kinyamwezi.

Wasukuma ni kabila kubwa kutoka eneo la kusini na mashariki ya Ziwa Viktoria, nchini Tanzania. Kabila hili hasa huishi katika mikoa ya Mwanza na Shinyanga. Mwaka 2001 idadi ya Wasukuma ilikadiriwa kuwa 3,200,000 [1]. Lugha yao ni Kisukuma. Kisukuma ni miongoni mwa lugha za Kibantu ambazo hubainishwa kama lugha mabishi.

Wayao ni kabila kutoka eneo la kusini ya Ziwa Nyasa. Mwaka 2001 idadi ya Wayao ilikadiriwa kuwa 1,942,000, ambao 1,000,000 wanaishi Malawi, 450,000 ni wakazi wa Msumbiji, na 492,000 wako Tanzania [1]. Lugha yao ni Kiyao.

Wazanaki ni kabila kutoka eneo la kaskazini-magharibi ya nchi ya Tanzaniai,

Wazaramo ni kabila kutoka eneo baina ya Dar es Salaam na Bagamoyo, nchini TanzaniaWazaramo ni sehemu ya Wabantu. Mababu wanaaminika waliingia katika eneo la Tanzania katika milenia ya kwanza. Historia yao ya kimdomo inasema ya kwamba walihamia pwani katika mazingira ya Daressalaam kutoka Uluguru (Morogoro) katika karne ya 18.

Walipokaa kwenye pwani walikuwa karibu na makazi ya Waswahili wakaanza kufaamiana na Uislamu. Taarifa za wakoloni Wajeruami mwanzoni wa karne ya 20 zinaonyesha ya kwamba wakati ule Uislamu ulikuwa umeenea kati ya Wazaramo na waliendelea kujiunga nayo haraka [2]. Siku hizi idadi kubwa wa Wazaramo ni Waislamu.

Makabila Mengine Ni Haya Hapa Chini

Wakabwa,Wazigula,Wazinza,Wazyoba,Wahadzabe (pia wanaitwa Watindiga),Wahangaza, Wakahe,Wakami,Wakara (pia wanaitwa Waregi),Wakerewe,Wakimbu,Wasumbwa,Waswahili,Watemi(piawanaitwaWasonjo),Watongwe,Watumbuka,Wavidunda,Wavinza,Wawanda,Wawanji,Waware(inaaminikalughayaoimekufa),,Wanyanyembe,Wanyaturu(piawanaitwaWarimi),Wanyiha,Wapangwa,Wapare(piawanaitwaWasu),Wapimbwe,Wapogolo,Warangi(auWalangi),Warufiji,Warungi,Warungu(auWalungu),Warungwa,Warwa,Wasafwa,Wasagara,Wasandawe,Wasangu,Wasegeju,Washambaa,Washubi,Wasizaki,Wasuba, Wanyambo,Wanyamwanga, ,Wandonde,Wangasa, ,Wandali,Wandamba,Wandendeule, .Wangindo,Wangoni,Wangulu,Wangurimi (au Wangoreme),Wanilamba (au Wanyiramba),Wanindi,Wamakua (au Wamakhuwa),Wamakwe(piawanaitwaWamaraba),Wamalila,Wamambwe,Wamanda,Wamatengo,Wamatumbi,Wamaviha,Wambugwe,Wambunga,Wamosiro,Wampoto,Wamwanga, ,Wamagoma, ,Wakutu,Wakw'adza,Wakwavi,Wakwaya,Wakwere (pia wanaitwa Wanghwele),Wakwifa,Walambya, Wakisankasa,Wakisi,Wakonongo, Wagorowa (pia wanaitwa Wafiome),Wagweno, Waikizu,Waikoma,Wairaqw (pia wanaitwa Wambulu),Waisanzu,Wajiji

Tuesday, July 20, 2010

umeshawahi kupata mtoto kama huyu?

dunia ina maajabu lakini haya ni ukweli tupu si tu watoto wakibongo wanaweza kucheza ndombolo bali hata huko ughaiguni mambo haya wanayaweza, ukitaka kufahmu hilo hebu cheki hapo kwenye play then uone dogo anavyoyaruka majoka,,,,,,,,,,,,,,,kweli huyu ni full msanii,nyota njema huonekana asubuhi msemo ni mashuhuri sana unathibitishwa na video gonga hapo na ujionee mwenyewe..............
WELCOME TO KUNAMBI BLOG!!!
Miongoni mwa miji inayokua kwa kasi duniani moja wapo ni jiji la Dar es salaam,Maarufu sasa kamam jiji la Lukuvi,mji huu unapanuka kwa kasi sana hususani katika shughuli za kimaendeleo,kisiasa na kijamii,lina wakazi wake wanafahamika kwa kabila la wazaramo yumkini lina makabila tofauti kama sio yote yanayopatikana nchi nzima ya Tanzania,jiji hilo lina wakazi wapatao takriban zaidi ya milioni 5,lina wilaya zipatazo tatu, Temeke,Ilala na Kinondoni,uchumi wa jiji hili unategemea sana shughuli za maofisini na biashara za hapa na pale,miundombinu ya jiji hili bado ni tabu kidogo japokua serikali inafanya kila jitihada za kuhakikisha mambo yanaenda sawa, jiji hili lina shughuli nyingi sana ikiwemo biashara,uvuvi,utalii,nk na kuna baadhi ya sekta tofauti zinazopatikana ndani ya jiji la Mh Lukuvi,kwa ufupi hilo ndilo jiji la Da res salaam au wajanja wanaliita jiji la Bongo,maana ukitaka kuishi ndani ya bongo lazima utumie ubongo vilevile,

Monday, July 19, 2010

Kunambi

shuhudia mtoto huyu akicheza mambo ya wakawaka bofya kwenye play hapo kujionea mwenyewe.
Mr Kunambi Junior anaribisha maoni

Sunday, July 18, 2010

barabara za lindi na mtwara,kipande cha kilometa sitini na mbili mbioni kwisha.

magari yakiwa yamenasa katika kijiji cha nyamwage barabara ya kwenda Lindi/Mtwara,eneo hili inapofika kipindi ni bora tu usisafiri kwa sababu pindi mvua zinapoanza barabara inakua haipitiki abiria wanalala porini siku mbili hadi tatu au wiki nzima,juhudi za kumaliza kipande hiki cha ujenzi wa barabara hii ipatayo kilometa 62 inaendelea huku mkangarasi aliyepewa jukumu la kukamilisha kipande hicho akiwa katika hatua ya mwisho ya kumaliza kujenga makalavati na madaraj,pindi tu barabara hii itakapokwisha itawarahishia wakazi wa miji hiyo ya kusini kufanya shughuli zao kwa urahisi zaidi,
jamani uoneni barabara zetu za lindi na mtwara kero tupu!!!!1

Kunambi Jr

am Tanzanian citizen,age 28 and a holder of advance Diploma in Information Technology, graduated at The Institute of Finance Management (IFM).